.

Tuesday, July 19, 2011

NJAA SOMALIA INAZIDI KUTISHIA............


Hali ya njaa katika nchi ya Somalia inazidi kuwa mbaya na Umoja wa mataifa umelenga kutangaza kuwa sehemu kadhaa nchini humo zinakabaliwa na janga la kimataifa kufuatia hali hiyo.


Maelfu ya familia yapo katika hali mbaya ya uhitaji wa chakula na maji na wanatembea mwendo mrefu kutoka nchini Somalia mpaka katika makambi ya wakimbizi ya Dadaab huko  mashariki mwa Kenya.






Hali ya ukame iliyolikumba eneo hilo haijawahi kuonekana kwa zaidi ya miaka 60 na umoja wa mataifa umeielezea hali hiyo kuwa ni eneo la dharura kwa binadamu.

Wakati huo huo Umoja wa Mataifa umesema kuwa mashirika ya kutoa misaada yanahitaji kupata hakikisho zaidi kutoka makundi ya wapiganaji kabla kupeleka misaada nchini humo.

No comments:

Post a Comment