.

Friday, April 29, 2011

PICHA ZAIDI KUHUSU HARUSI YA KIFALME
In this image taken from video, Britain's Prince ...
inawezekana kina dada wengi walikuwa wanamtamani lakn wapiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
Prince William, Kate Middleton, Kate, Duchess ...
mambo ya Duke Of Cambridge
   
 .
Britain's Prince William kisses his wife Kate, ...
jamani jamani jamaniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
Kate Middleton, Michael Middleton, Pippa Middleton
Heshima lazima iwepooooooooooo
Britains Prince William and his wife Catherine, ...
Gari hii ilitumiwa pia na prince charles na mkewe marehemu princes diana mwaka 1981 ambao ni wazazi wa prince william wakati wa harusi yao,imetumiwa pia na prince william na mkewe cate
 

PWEZA IKER ATABIRI USHINDI MECHI YA MARUDIANO KATI YA MADRID NA BARCELONA

Pweza aliyepewa jina la Iker wa nchini Hispania ametabiri kuwa Real Madrid wataigaragaza Barcelona na hatimaye kufanikiwa kucheza fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya.
Pweza huyo ambaye awali utabiri wake kwa mechi mbili za wababe hao wa Hispania ulikuwa wa kweli, ametabiri kwa mara nyingine kuwa Real Madrid watafanikiwa kuitoa Barcelona kwenye mechi za nusu fainali ya kombe la mabingwa ulaya.

Pweza huyo aliyepewa jina la Iker kwa heshima ya golikipa mkongwe wa Real Madrid, Iker Casillas alitabiri mechi mbili zilizopita za watani hao wa jadi ambapo ya kwanza walitoka sare ya 1-1 wakati mechi ya pili Madrid walishinda 1-0.

Pweza huyo mwenye uzito wa kilo 16 aliwekwa kwenye Aquarium kwenye mji wa Benalmadena uliopo kusini mwa Hispania ambapo alikimbilia kwenye sanduku lenye bendera ya Real Madrid na kuliacha sanduku lenye bendera ya Barcelona. Masanduku yote mawili yalikuwa na chakula kwaajili ya kumvutia Pweza huyo.

Madrid na Barcelona wanapambana kesho jumatano kwenye mechi ya kwanza ya nusu fainali itakayochezwa kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu wakati mechi ya marudiano itakuwa kwenye uwanja wa Barcelona, Nou Camp mnamo mei tatu.

Timu itakayofanikiwa kumtoa mwenzake itakutana na mshindi kati ya Manchester United ya Uingereza na Schalke 04 ya Ujerumani.

WAMJUA MTU MFUPI KULIKO WOTE DUNIANI?

Junrey Balawing huenda akatangazwa mtu mfupi kuliko wote duniani mwezi juni mwaka huu atakapotimiza umri wa miaka 18 akiwa na urefu wa sentimita 56 tu. GONGA Life Style Pembeni Kushoto kwa habari zaidi.

YAWEZEKANA BABA KUMUOMBA MWANAYE MSAMAHAA?

Katika mazingira ambayo tunakulia sisi watanzania mara nyingi mama ndio anakuwa karibu na watoto zaidi kuliko baba. Ofcourse hii inaweza kubadilika kutegemea na familia husika. Ila kwa mtazamo wa ujumla naweza kusema hivi ndivo ilivyozoeleka. Sasa mara nyingi baba anakuwa mkali kwa watoto inafikia hatua mtoto akimuona baba amerudi kutoka kazini badala ya kufurahia ndio anasikitika. Anamsalimia then anatafuta sehemu ya kujificha. Well, hili si tatizo sana maana sometime inakuwa ni nature ya mtu kwamba anakuwa yupo hard kwa kila mtu hata kwa familia yake.

Sasa tatizo linakuja pale huyu baba ambaye hana ukaribu na wanae pale anapojikuta amemchapa mwanae kimakosa au kampiga kimakosa then kwa sababu yupo too superior anaona kuomba msamaha kwa mwanae ni udhaifu. Akijiangalia kwa jinsi anavyo behave then aseme samahani....anaona duh hii nitakuwa nimejishusha hadhi yangu. Anaamua kunyamaza tu na kuendelea na maisha kama kawaida.

Sasa ubaya wake ni kwamba mtoto nae anakulia katika mazingira kama hayo. Hajafundishwa kuomba msamaha na hajawahi kuombwa msamaha. Hali hii inakuwa inaendelea kutoka kizazi hadi kizazi. Mimi sidhani kama ni aibu au kujidhalilisha kama ukiamua kuomba msamaha pale unapofanya makosa hata ka wale waliokuzidi umri. Ndio inakuongezea heshima maana binadamu mara nyingi tunakumbukana kwa mabaya so watu wanapokuzungumzia pale ulipochemsha basi watasema pia kuwa uliomba msamaha. Mimi kwa mtazamo wangu nadhani ndio inaongeza utu wako mbele za watu.

Anyway point ya muhimu niliyotaka kuisema ni kwamba mara nyingi kuomba msamaha kwa mwanao inakauwa ni vigumu zaidi kama utatengeneza umbali kati yako na watoto wako. Ikishakuwa hivyo kama ukimfanyia makosa mwanao kuomba msamaha inakuwa ni kazi ngumu sana. Kuna familia moja naifahamu ambayo baba na mama huwa wanashindana kutengeneza ukaribu na watoto wao hali ilinivutia sana sio siri. Hope kwamba we can adopt some ways of living from other families. Hii haimaanishi kuwa upo dhaifu. Kwa sababu be sure kwamba zipo pia familia ambazo pia zina adopt some ways of life from you
.

"DINGI AKINISTUKIA SIJUI ITAKUAJE?"

NI KWELI MAENEO YETU YANANUKA?

"JAMANI TUSISUBIRI MVUA ZIKATIKE HALAFU TULALAMIKE NJAA"

UKIMUONA AKIWA ANAENDA OFISINI ANAJIHESHIMU SANA LAKINI!!!!!!!!!!!!!!!!!!



Hapa akiwa maeneo yake ya home


"SIJALALA NAKUSANYA NGUVU ZA KUKATA MAJANI"

  Bwana Frank akiwa amejipumzisha kabla ya kuanza kukata majani maeneo ya Ilala. Yawezekana kabisa jamaa amesahau ule msemo "USIFUGE WANYAMA MJINI" maana hawatapata malisho mazuri kama vijijni, huku mjini watakula lami.

"HUKU KWETU ZINA SOKO SANA TUPE FURSA TUJE TUWEKEZE NA KWAKO"


JK akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wamafunzi
wanaosoma katika vyuo mbali mbali nchini Misri baada ya kukutana na kuzungumza nao mjini Cairo.
JK alionesha kufurahiswa na juhudi zao walizo zionesha na kujitolea kompyuta 6 na amehadi kuwasidia zaidi hapo baadae, JK alitoa mchango mara tu baada ya kusomewa risala ya wanafunzi iliyosomwa na katibu mkuu wa unoja huo ND. Gharibu nasro, ndani ya risala hiyo waliomba serekali inayo ongozwa na JK kujenga kituo cha utamadu nchi humo na Raisi aliwahidi kulifanyia kazi.