.

Wednesday, July 20, 2011

AWAUA WAZAZI WAKE NA KUANGUSHA PARTY NYUMBANI



Kijana mmoja wa kiume katika jimbo la Florida nchini Marekani anatuhumiwa kuwauwa wazazi wake kwa kuwapiga nyundo na kisha akafanya tafrija yaani party amefikishwa mahakamani.

Kijana huyo ambaye ametambuliwa kwa jina la Tyler Hadley, mwenye umri wa miaka 17 anatuhumiwa kuwauwa wazazi wake Blake na Mary-Jo Hadley siku ya jumamosi na kisha akawafuingia miili hiyo chumbani na kuwaalika wageni  katika hafla hiyo.

Amefunguliwa mashitaka kama mtu mzima lakini hatahukumiwa kifungo cha kifo kwa kuwa umri wake ni mdogo na chanzo cha mauaji hayo bado hakijajulikana.

''MAMA G'' KUNG'ARA KATIKA FILAMU MPYA.......


Mwigizaji nyota wa filamu nchini Nigeria Patience Ozokwor maarufu kama '''Mama G'' anatarajiwa kushiriki katika filamu mpya nchini Malawi iitwayo ''The Return''.

Katika filamu hiyo Mama G kama kawaida yake ataigiza kama mama mwenye roho mbaya anayewatesa watoto yatima na kuwatumikisha kazi watoto hao kwa ajili ya kujiongezea kipato.


Mama G pia anatarajiwa kufanya ziara kwa kutumbuiza live stejini katika miji mitatu ikiwemo Lilongwe,Blantyre na Mzuzu.

TREY SONGZ NDANI YA MOVIE KALI............


Nyota mkali Trey Songs amesaini mkataba wa ku-act kama starring kwenye remake ya movie ya kutisha iitwayo ''Texas Chainsaw Massacre'' itakayokua katika mfumo wa 3D....


Texas Chainsaw Massacre ilitengenezwa mwaka 1974 chini ya Directer John Lussenhop (aliyengeneza pia movie kali ya movie Takers,na Trey Songz humo ndani ame-act kama boyfee wa mdada Alexandra Daddario Movie hiyo inatarajiwa kuanza kutengenezwa mwezi huu pande za Shreveport, Lousiana na inatarajiwa kuwa kwenye theaters mwakani mwezi October,2012

SWIZZ BEATZ KUMSAIDIA RAFIKI YAKE DMX


Produza mkali Swizz Beatz ameamua kumfikia rafiki yake DMX kwa kumpa ofa ya kumsaidia rapa huyo aliye matatani kurejea tena katika gemu baada ya kuachiwa huru kutoka gerezani siku ya Jumanne.



DMX ambaye jina lake halisi ni Earl Simmons aliachiwa jela kutoka gereza la Arizona baada ya kutumikia kifungo cha miezi saba, kutokana na kukiuka masharti ya kuwa chini ya uangalizi, lakini sasa anataka kurejea studio baada ya kukutana na familia yake.

Nyota wa hip hop Swizz Beatz ambaye ni mshirika wa karibu wa DMX, pia ni memba wa kundi la Ruff Ryders amesisitiza kuwa anamgojea DMX kumpigia simu ili warejee tena mzigoni.

MODEL AKANUSHA KUTOKA NA JLO...........



Model ambaye ameshiriki katika video mpya ya Jennifer Lopez amekanusha uvumi kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na mwanamuziki huyo ikiwa ni siku chache tu kupita tangu atengane na mumewe.


Model huyo aliyetamba katika tamthilia ya ''don't mess with an anjel'' huyo William Levy maarufu kama Juan Miguel au Brad Pitt wa Cuba anaonekana katika video hiyo akiwa kimahaba ufukweni na J-LO huku akimbambia katika video ya wimbo wa I'm Into You.


Levy alitengana na mkewe Elizabeth Gutierrez mwezi mmoja baada ya kushutiwa video hiyo Aprili mwaka huu ambapo J-Lo naye ametangaza kutengana na mumewe Marc Anthony Ijumaa ya wiki iliyopita.