.

Tuesday, July 19, 2011

MWANDISHI WA HABARI UINGEREZA AKUTWA AMEKUFA

Mwandishi wa zamani wa gazeti maarufu duniani la News Of The World (NOTW) Sean Hoare ambaye alivujisha kashfa iliyoliyolikumba gazeti hilo kujihusisha kunasa simu za watu mbali mbali amekutwa amekufa nyumbani kwake nchini Uingereza.

Polisi nchini imesema mwili wa Hoare ulikutwa nyumbani kwake huko Watford siku ya Jumatatu asubuhi baada ya wasiwasi kuibuka kwa kutofahamu alipo na msemaji wa polisi wa kituo cha Hertfordshire amesema kifo hicho kinachukuliwa kama hakieleweki.

Hoare alidai katika makala yake kupitia gazeti la New York Times kuwa Andy Coulson ambaye kwa sasa ni msaidizi wa waziri mkuu wa Uingereza alimshawishi kunasa mawasiliano ya simu.

No comments:

Post a Comment