.

Friday, July 22, 2011

MODEL WA JLO NDANI YA SCANDAL YA NGONO.............


William Levy model kutoka nchini Cuban ambaye alihusishwa kimahaba na mwanamuziki Jennifer Lopez baada ya kutangaza kuachana na mumewe hivi sasa yupo katikati ya skendo ya ngono.


Mwigizaji uyo nyota maarufu kama Juan Miguel ambaye alicheza kama mpenzi wa Jlo katika video ya ''Into You video'' hivi sasa anapamba vichwa vya habari kwa kukabiliwa na tuhuma za kujihusisha na mahusiano na binti wa miaka 17 mwaka jana ambapo binti huyo ametoa tuhuma kuwa Levy alimlazimisha kufanya naye ngono katika chumba cha hoteli na anadai dola milioni 2.5 kwa uharibu aliofanyiwa.

RIHANNA ASIKITISHWA NA KIFO CHA FAN WAKE...........


Mwanamuziki Rihanna ameguswa na kifo cha shabiki wake kijana aliyefariki kwa ajali ya gari huku akisikiliza nyimbo zake ambapo mkali huyo wa kibao Umbrella alichanganyikiwa baada ya kubaini shabiki yake huyo Karen mwenye miaka 17, anaye miliki kurasa maalum ya twitter kwa ajili ya Rihanna amefariki katika ajali.


                                      
                                           
Rafiki wa kijana huyo alimuhabarisha Rihanna kuhusiana na tukio hilo kupitia  kwenye tuvuti ya jamii na ndipo Rihanna alipoandika ujumbe wa rambirambi uliosema shabiki wangu mkubwa amefariki dunia hii leo akiwa na umri mdogo, Karen umetutoka hatutakusahau daima.

R.KELLY APATA NAFUU



Nyota wa muziki wa soul R. Kelly ameanza kupata nafuu huko Chicago, katika hospitali Illinois baada ya kufanyiwa upasuaji wa dharura kwenye koo lake.


Mwimbaji huyo wa kibao cha I Believe I Can Fly alikuwa na tatizo katika mfumo wa koo kuanzia jumanne ya wiki hii ambapo msemaji wake Allan Mayer amebainisha kuwa R. Kelly ataendelea kulazwa katika hospitali hiyo ya Kaskazini Mashariki mwa Chicago kwa muda usiojulikana.

KATTY PERRY AONGOZA TUZO ZA MTV BASE...................


Nyota wa muziki wa Pop nchini Marekani Katy Perry anaongoza katika tuzo za mwaka huu za MTV base kwa kuteuliwa kuwania tuzo hizo katika vipengele tisa ambapo baadhi ya tuzo anazowania ni pamoja na video bora ya mwaka, video bora ya Pop pamoja na video yenye best special effects.


 
Mwanumuziki kutoka nchini Uingereza Adele pamoja na Kanye West wameteuliwa kuwania tuzo kwenye vipengele saba ambapo wasanii wengine walioteuliwa zaidi ya mara moja ni Lady Gaga, Beyonce pamoja na Bruno Mars.




Katty Perry anatamba na ngoma kali kama "California Gurls" na "Teenage Dream"anaweza kunyakua tuzo kibao katika vipengelea alivyochaguliwa.