.

Thursday, July 21, 2011

CHRIS BROWN APATA DILI LA MOVIE........


Nyota wa R&B kutoka nchini Marekani Chris Brown anatarajiwa kuonekana katika filamu mpya ya vichekesho itakayotokana na story iliyoandikwa na Steve Harvey kwenye kitabu chake cha Ac Like a lady,Think like man ambacho kilikuwa kitabu chenye mauzo ya hali ya juu.


Filamu hiyo inatarajiwa kuwa na jina la ''Think Like a man'' ambayo pia itawashirikisha waigizaji kama Kevin Hart,Michael Ealy,Gabrielle Union,Regina Hall,Lala Vasques na 'Entourage' Jerry Ferrara.

RIHANNA AKIKATA MITAA NA KIVAZI CHAKE.................


Mwimbaji wa R&B Rihanna amejikuta akiwaacha wakazi wa New Jersey Marekani mshanga kutokana na kuvaa kivazi cha mitego na kutembea nacho mtaani.


Nyota huyo anayetamba na kibao cha S&M  alionekana akikata mitaa bila wasiwasi wakati wengine walidai alikuwa anatafuta chumba cha kulala lakini hakuweza kulala hapo na badae kurejea jijini New York.