.

Tuesday, July 19, 2011

LADY GAGA AKABILIWA NA WAHALIFU WA MTANDAO


Nyota wa muziki nwa mwanamapinduzi wa mitindo ambaye haishiwi vituko Lady gaga amewaita polisi baada ya wahalifu wa mtandao ''maharamia'' kuishambulia tovuti yake binafsi na kuiba taarifa za mashabiki wake.

Tovuti hiyo ya Gaga imevamiwa na maharamia hao wa mtandao ambao wamechukua taarifa za siri za mashabiki zikiwemo majina yao na anuani za barua pepe zao.

Wawakilishi wa Lady Gaga wamesema wahalifu wameiba taarifa zilizokuwepo kwenye database ya tovuti zikiwemo za majina yote mawili ya baadhi ya mashabiki wa msanii huyo.

No comments:

Post a Comment