.

Friday, August 12, 2011

BREAKING NEWZZZZZZZ!!!!!!!BP YASIMAMISHWA.....!!!!!!


BP yasimamishwa, bosi wake kushitakiwa
HATUA ZINAZOCHUKULIWA

    Baada ya kuchambua kwa undani kuhusu suala hili, Bodi ya Wakurugenzi imekutana leo na kuamua yafuatayo:

    a) Kuziandikia ONYO KALI kampuni za Oilcom (T) Ltd, Camel Oit (T) Ltd na Engen Petroleum (T) ltd kuwaonya kutorudia tabia walioionesha ambayo ni kinyume na Sheria za Tanzania na kuwaagiza wauze mafuta kwa watu wote bila ubaguzi. Amri hii itafuatiliwa kwa ujirani na ikibainika wamekiuka hatua kali zaidi zitachukuliwa dhidi yao mara moja

    b) Kusitisha leseni ya biashara kwa BP (T) Ltd kwa MIEZI MITATU KUANZIA LEO kuuza mafuta ya Petroli, Dizeli na Taa.

    c) BP (T) Ltd ataruhusiwa kuendelea kuuza mafuta ya ndege kutokana na ukweli kwamba EWURA haidhibiti bei za mafuta ya ndege ambao ndio msingi wa mgomo kwa wafanyabiashara ya mafuta.

    d) Pia BP (T) Ltd ataruhusiwa kuuza mafuta yake yote ya petroli, dizeli na taa yaliyopo kwenye maghala yake kwa wafanyabiashara wengine wa jumla kama wanataka kwa usimamizi wa EWURA ili kuzuia kutoharibika kwa mafuta hayo katika kipindi hicho cha miezi mitatu ambapo hataruhusiwa kufanya biashara ya mafuta ya jumla.

    e) Hata hivyo, vituo vyote vya rejareja (Petrol Stations) vya vyenye nembo ya BP vitaruhusiwa kuuza mafuta kwa kununua mafuta kwa wafanyabiashara wengine wa jumla na si kwa BP.

MERCY JOHNSON MJAMZITO........!!!!!???

Utata umeibuka kwa mmoja wa waigizaji wa sekta ya filamu ya Nigeria Mercy Johnson kuhusiana na mpango wake wa kuoana na Prince Odianosen Okojie ambaye tayari ana mke mwingine.

Licha ya sababu kadhaa zilizotolewa kuna habari mitaani kuwa sababu kubwa ya Mercy Johnson kung'ang'ania ndoa hiyo ni ujauzito alionao.

Inasadikiwa kusitisha ndoa hiyo wakati huu ambapo anaujauzito wa mchumba wake huyo na hali hiyo ndio chanzo cha yeye kukabiliwa na mtafaruku huo wa kuolewa na mume wa mtu.

OLIVER MTUKUDZI AWASILI KAMPALA..........

Msanii wa kimataifa raia wa Zimbabwe Oliver Mtukudzi amewasili Jijini Kampala  kwa tamasha maalum la kuwasaidia wagonjwa wa saratani.

Mtukudzi atafanya onyesho hilo leo jioni Jijini Kampala pamoja na mwanamuziki Suzanne Awiyo.

Mtukudzi akiwa na Suzan Awino

Kwa mujibu wa waandaaji tamasha hilo fedha zitakazopatikana zitatolewa kwa wagonjwa wa saratani wa taasisi ya Bless A Child Foundation.