.

Tuesday, July 19, 2011

AISHA MADINDA HUYOOO KWA CHOKI.....



Aliyekuwa mnenguaji mahiri wa bendi ya African Stars wana wa kutwanga na kupepeta Aisha Madinda amehamia rasmi bendi ya Extra Bongo kwa Mzee wa farasi Ally Choki na kuungana na mwalimu wa madansa Super Nyamwela kusongesha mzigo katika bendi hiyo inayokuja kwa kasi ya ajabu katika muziki wa Dansi Tanzania.





Kuna habari kuwa aliyekuwa mshindi wa kimwana manywele wa twanga pepeta kwa mwaka 2011 amechukua nafasi yake kwenye bendi hiyo kutokana na umahiri wake wa kudance.

No comments:

Post a Comment