.

Tuesday, July 19, 2011

50 CENT KUSAIDIA WENYE SHIDA



Rapa 50 Cent ana nia ya kutumia nafasi yake pamoja na ushawishi alionao katika jamii kuwasaidia wenye shida na tayari ameshajiwekea lengo la kuwalisha waafrika bilioni moja.

Mkali huyo wa muziki warap ulimwenguni alibadili maisha yake kutoka uuzaji wa dawa za kulevya Jijini New York na kuwa miongoni mwa wasanii wakali wa hip hop na kupata pesa nyingi tangu mwaka 2003.


Na sasa nyota huyo wa muziki wa hip hop anataka kugawana na wenye shida kipato chake kwa kutilia mkazo ndoto yake ya kuwasaidia watu wenye njaa barani Afrika.

No comments:

Post a Comment