.

Tuesday, May 10, 2011

"MATAJIRI MJIANDAE KWA KIBANO.

WAZIRI Kivuli wa Fedha na Uchumi, Zitto Kabwe amesema katika Bajeti ijayo ya Serikali, atapendekeza matajiri wabanwe ili kupunguza makali ya maisha kwa Watanzania walio wengi ambao kwa sasa wanataabika kutokana na umaskini.

Alisema hayo jana wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Mbarali, mjini Rujewa, akisisitiza kuwa hiyo ndiyo njia pekee ya kutatua matatizo ya ugumu wa maisha yanayowakabili Watanzania.
"Tofauti ya kipato Tanzania inakuzwa na sababu mbili, moja ni matajiri kuzidi kuwa matajiri na maskini kuendelea kuwa maskini, hivyo hatua za kisera zinapaswa kuchukuliwa kuwazuia maskini kuwa maskini zaidi kwa kuwapunguzia gharama za maisha," alisema Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema).
Alisema katika Bajeti ijayo, atapendekeza kuziba pengo la kodi kwa kupandisha kodi ya kampuni kufikia asilimia 35, kuuza hisa za serikali katika kampuni za Airtel, NBC na BP hivyo kupunguza misamaha ya kodi hadi kufikia asilimia moja ya pato la taifa
.

No comments:

Post a Comment