.

Tuesday, May 10, 2011

NOELLE AUZA BIKIRA YAKE KWA SHILINGI MILIONI 100.

Mwanafunzi mmoja wa kike wa nchini Ubelgiji mwenye umri wa miaka 21 ameinadi bikira yake na kufanikiwa kupata mteja aliyeinunua kwa takribani Tsh. Milioni 100.
  Mwanafunzi huyo aliyejulikana kwa jina moja la Noelle aliunadi mwili wake kwenye mnada wa tovuti ya Yantra ya mjini Amsterdam, Uholanzi ambayo inadili na kuwatafutia wanaume wanawake.

Noelle ambaye ni mwanafunzi anayeishi nchini Ubelgiji, aliamua kuinadi bikira yake nchini Uholanzi huku akificha sura yake ili wazazi wake na marafiki zake wasimgundue.

Baada ya miezi miwili ya mnada huo hatimaye mnada huo umeisha kwa Noelle kufanikiwa kuiuza bikira yake kwa euro 50,000 ambao ni zaidi ya Tsh. Miloni 105.

Noelle atatumia masaa 24 na mwanaume aliyeshinda mnada huo ambaye hajataka kujitambulisha.

Mwanaume huyo mbali ya kupata nafasi ya kuivunja bikira ya kimwana huyo atatakiwa kama sharti la mnada huo ampeleke Noelle kwenye mgahawa wowote ambao Noelle atauchagua.

Noelle anasema kuwa mshindi wa mnada huo atapewa cheti cha daktari kinachothibitisha kuwa Noelle ni bikira. Noelle alisisitiza kuwa tendo la ngono lazima lifanyike kwa kutumia kondomu.

Noelle alidai kuwa aliamua kuinadi bikira yake ili aweze kupata pesa za kujikimu kwenye masomo yake.

Noelle alijinadi kwenye mnada huo kwa kusema kuwa yeye ni mrembo mwenye macho ya hudhurungi, urefu wa mita 1.73, kiuno cha saizi 10 na matiti ya saizi B.

"Mimi ni msichana wa kawaida na wazazi wangu hawatafurahia wakisikia ninainadi bikira yangu", alisema Noelle.

Bei ya kuanzia kuweka dau katika mnada huo ilikuwa ni euro 5,000 (Tsh. Milioni 11).

Katika kuwadhirihishia watu kuwa yeye si kahaba, Noelle alidai kuwa atatoa asilimia tano ya pesa atakazozipata kwa mashirika ya hisani.

No comments:

Post a Comment