.

Tuesday, May 10, 2011

HUU SASA UBAGUZI WA RANGI.

Waziri wa michezo wa Ufaransa amemwondolea lawama kocha wa timu ya taifa ya soka nchini humo Laurent Blanc kuhusiana na ubaguzi wa rangi, baada ya kocha huyo kupendekeza kupunguza idadi ya wachezaji weusi katika timu ya taifa.
Waziri huyo, Chantal Jouanno amesema hakuna ushahidi kwamba Blanc alivunja sheria yoyote kwa kujadili kupunguza idadi ya wachezaji weusi na wale wenye asili ya Afrika Magharibi, wanaojumuishwa katika timu za vijana za Ufaransa.
Blanc amejitetea kwamba alieleweka vibaya.
Kocha huyo pamoja na makocha wengine wa timu za vijana walikuwa wanajadili jinsi ya kuwazuia kwenda kuchezea nchi zingine wachezaji wanaokuzwa nchini Ufaransa.
Bi Jouanno amesema hatma ya mkurugenzi mkuu wa mafunzo katika timu ya taifa Francois Blaquart ambaye alisimamishwa kazi kufuatia kujitokeza kwa habari hizo itaamuliwa na shirikisho la soka la Ufaransa (FFF).
Shirikisho hilo lilitazamiwa kutoa taarifa za uchunguzi wake Jumanne alasiri.
Mapendekezo hayo yamezua tafrani katika shirikisho la soka la Ufaransa, ikiwa bado haijapita mwaka tangu Laurent Blank alipoajiriwa kujenga upya timu ya taifa, baada ya matokeo mabaya kwenye mashindano ya Kombe la Dunia mwaka uliopita nchini Afrika Kusini.
Wavuti wa taarifa za uchunguzi wa kisiri- Mediapart, ulichapisha taarifa kudai Blaquart alipendekeza kupunguzwa kisiri idadi ya wachezaji weusi na wale wenye asili ya Afrika Magharibi hadi kubakia asilimia 30 kwenye baadhi ya vituo vya kutoa mafunzo kwa vijana chipukizi, kikiwemo kituo mashuhuri cha Clairefontaine.
Ilidaiwa Blanc alikubaliana na mpango huo ili kukuza zaidi wachezaji wenye ''utamaduni na histoaria'' ya Wafaransa.
Wakati wa Kombe la dunia wachezaji wapatao tisa katika timu za nchi zingine walikuwa ambao waliwahi kuichezea timu za taifa za vijana nchini Ufaransa.

No comments:

Post a Comment