.

Friday, May 6, 2011

WANA NDOA SOMENI HII.

Mwarabu mmoja wa Dubai amefikishwa mahakamani na mkewe na kufunguliwa madai ya fidia ya dola milioni 12.25 kwa kushindwa kumfikisha kileleni mkewe kwenye mambo ya malavi davi na hivyo kumsababishia mkewe mawazo mengi na kumchanganya akili.
Mke wa mwanaume huyo ambaye hakutajwa jina lake aliiambia mahakama kuwa mume wake alikuwa akizua sababu mbalimbali kumnyima unyumba kwa miezi minne ya mwanzo ya ndoa yao iliyofungwa mwaka 2008.

Mwanamke huyo aliendelea kusema kuwa baadae aligundua kuwa mumewe hawezi kazi kitandani kwani alikuwa akisumbuliwa na tatizo la uume wake kutosimama 'dede' hata aimbiwe nyimbo gani, limeripoti gazeti la Gulf News.

"Kwa kuangalia misingi ya tamaduni za kiarabu na jinsi mwanamke anavyochukuliwa katika jamii, niliamua kukaa kimya na kujaribu kuizoea hali hii huku nikiomba Mungu mambo yawe sawa", alisema mwanamke huyo.

Mwanamke huyo aliiambia mahakama kuwa mumewe ameshindwa kumtimizia mahitaji yake.

Aliendelea kuiambia mahakama kuwa mumewe alimsimamisha kazi kabla ya kumuoa na alimvua vidani vyake alivyokuwa navyo wakati huo.

Mwanamke huyo anadai fidia ya dirham milioni 45 ambazo ni sawa na dola milioni 12.25 kama fidia ya mumewe kumchanganya akili na kumsababishia mawazo mengi kwa kutomtimizia mahitaji yake.

No comments:

Post a Comment