.

Friday, May 6, 2011

KWELI PALICHIMBIKA.

Picha hizi za kutisha za maiti za watu waliouliwa ndani ya nyumba ya Osama bin Laden unaweza ukaziona lakini picha za maiti ya Osama bin Laden mwenyewe hautaiona kamwe kwani rais Barack Obama wa Marekani ameishatangaza kuwa picha hizo hazitatolewa kamwe.
Picha hizi za kutisha zinaonyesha maiti za wapambe wa Osama bin Laden ambao waliuliwa wakati kikosi maalumu cha jeshi la Marekani kilipovamia nyumba ya Osama bin Laden na kumuua Osama bin Laden.

Picha hizi zilipigwa na maafisa usalama wa Pakistan ambao waliingia kwenye nyumba ya Osama bin Laden mapema asubuhi ya jumatatu baada ya Marekani kuvamia kwenye nyumba hiyo kumuua Osama bin Laden na kisha kuondoka na maiti yake.

Maafisa usalama wa Pakistan ambao hawakutaka kutaja majina yao walizipiga picha hizo na kisha kuziuza kwa gazeti la The Gurdian la Uingereza.

Shirika la habari la Reuters limethibitisha kuwa picha hizo ni za kweli na zilipigwa eneo la tukio.

Kuhusiana na picha ya maiti ya Osama bin Laden, Rais Barack Obama wa Marekani alisema kuwa picha hizo hazitaonyeshwa kamwe kwani zitasababisha mtafaruku na pia zitatumiwa na wapinzani wa Marekani kueneza propaganda za chuki.

Rais Obama alisema kuwa picha za maiti ya Osama bin Laden hazitatolwa na wala picha au video zake wakati akizikwa hazitatolewa lakini aliwahakikishia watu kuwa Osama ameuliwa kweli na kamwe hataonekana tena akitembea kwenye ardhi ya dunia hii.

Gonga linki chini kuona picha za hali ilivyokuwa ndani ya nyumba ya Osama bin Laden na picha maiti za watu waliokuwa ndani ya nyumba hiyo.

No comments:

Post a Comment