.

Monday, May 16, 2011

FREEMASONS YATUA TANZANIA.

UJIO wa Taasisi ya Freemasons nchini na kufanyika kwa mkutano wao jijini Dar es Salaam, umezua mjadala miongoni mwa Watanzani ambapo imedaiwa jamii hiyo imeiteka Dunia.
“Alama kubwa za Freemasons ni nyoka, nyota, minara mirefu, jicho na mwenge, kuna majengo mengi sehemu mbalimbali duniani ambayo yanajengwa na kuwekwa alama hizo bila wenyewe kujua au huku wakijua,” alisema mtabiri mashuhuri nchini Sheigh Yahaya Husein.

Akifafanua zaidi, mnajimu huyo alisema alama hizo zinawekwa kwenye noti, minara, nembo mbalimbali katika nchi tofauti bila wenyewe kujua au wakati mwingine wakiwa wanajua.

“Majengo mengi ya bunge yana minara juu kwa mfano hili la kwetu jipya pale Dodoma, au katika majengo ya mabunge ya Kenya, Ujerumani, Marekani, Canada, Romania, Hungary na Uingereza ambalo lina minara mingi sana, je mmewahi kuuliza kwanini yanajengwa hivyo?” Alihoji mnajimu huyo.

Alisema alama ya Freemasons ya nyoka inatumika katika taasisi nyingi za ndani ya nchi au za kimataifa, akatoa mfano wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na hata katika noti ya Tanzania ya shilingi mia tano.

“Kwenye noti alama za Freemasons zipo nyingi kwa mfano Dola za Kimarekani zina alama ya nyota na hata katika noti zetu hapa nyumbani ipo, imewekwa kitaalamu sana katika noti ya shilingi mia tano,” alisema.

Alipoulizwa kama Freemasons inahusika na dini ya mashetani, mnajimu huyo alisema anavyofahamu ni kuwa asili yao ni taasisi nyingine iliyokuwa ikiitwa Skull and Bones (Fuvu na Mifupa) ambayo ilikuwa ikiabudu mashetani na kutoa kafara ya damu
.
“Hili tunalisema kwani hata Babu yake Rais wa zamani wa Marekani, George Bushi aitwae Peasscot S. Bush aliyezaliwa mwaka 1895 na kufa 1972 alikuwa mwanachama, mnaweza kupata haya katika mitandao mbalimbali, siyo siri,” alifafanua na kuongeza kuwa Freemasons ina wanachama matajiri na kwamba ni nadra sana kukuta mlalahoi.

Hata hivyo, katika mahojiano na mwandishi mmoja wa gazeti moja nchini miaka mitatu iliyopita Kiongozi wa Freemasons Afrika Mashariki, Jayantilal Chande alisema taasisi yake haihusiki kabisa na dini ya mashetani kama watu wanavyofikiria na badala yake inajihusisha na kuhudumia jamii kimaendeleo katika nyanja mbalimbali.

No comments:

Post a Comment