.

Monday, May 16, 2011

"ETI FUSO ZA MBOE NI CHAKAVU?"

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Marando amesema kuwa chama ndicho kilichomwomba Mwenyekiti wake Freeman Mbowe awauzie magari hayo ambayo CCM inayaita chakavu, “Mimi mwenyewe nilihusika kumwomba Mbowe atupe magari yale, akakubali. Baada ya hapo Kamati Kuu iliunda kamati ya watu wanne chini ya makamu mwenyekiti Zanzibar Mohamed Issa kumwomba mwenyekiti akiachie chama magari hayo.
 Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA, Anthony Komu akasema magari hayo hayawezi kufananishwa na magari mengine ya FUSO yanayotembea mitaani kwa kuwa hiyo ni mitambo maalumu yenye vipaza sauti vyenye thamani ya shilingi milioni 222/= na majenereta matatu ambayo kila moja lina thamani ya shilingi milioni 47/=, “Katika magari hayo kuna vipaza sauti (Public addressing system 3 sets) zenye thamani ya dola za Marekani 148,000 (shilingi milioni 222), jenereta tatu kila moja  shilingi milioni 15.5 sawa na shilingi 47,000,000/=”

Komu alisema kila gari lina bodi maalumu yenye uwezo wa kubeba watu wasiopungua 12, jenereta moja kubwa, mafuta ya helkopta, jukwaa la kuhutubia na vifaa vya matangazo ambazo zote zimejengwa kwa shilingi milioni 48.4/=

No comments:

Post a Comment