.

Monday, May 16, 2011

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema dawa pekee ya kumaliza tatizo la umaskini uliokithiri miongoni mwa Watanzania wengi nchini ni kuondoa ukiritimba na ufisadi. Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama hicho Taifa, Wilfred Lwakatare, alisema hayo alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mgazini, Kata ya Kilagano, Wilaya Songea Vijijini, mkoani Ruvuma jana. Mkutano huo ni wa kwanza kati ya mikutano mitatu ya hadhara iliyofanywa na Lwakatare, uliofuatiwa na ule alioufanya katika kituo cha mabasi cha mjini Peramiho na katika Uwanja wa Shule ya Msingi ya Lilambo, Songea mjini.

Lwakatare ni miongoni mwa viongozi waandamizi wa Chadema walioko katika timu sita zinazoendesha operesheni maalum ya chama hicho nchini inayohusisha maandamano.

No comments:

Post a Comment