.

Wednesday, April 27, 2011

LIL WAYNE: NITASTAAFU NIKIFIKISHA MIAKA 35

Rapper mkali kutoka nchini Marekani,Lil Wayne ambaye amekuwa katika game tangu akiwa na umri wa miaka 15 tayari ameanza kuzungumzia kustaafu mara atakapofikisha umri wa miaka 35. Lil Wayne ambaye miongoni mwa wafuasi wake kupitia label yake ya  Young Money ni pamoja na Rapper mkali mzaliwa wa Toronto,Canada na rapper machachari wa kike,Nicki Minaj, hivi sasa ana umri wa miaka 28. Kwa maana hiyo Rapper huyo ana miaka mingine 7 tu kusimama imara katika ulingo wa muziki.
Akizungumza na Angie Martinez wa Hot 97, Lil Wayne ambaye mashabiki wake hupenda kumwita “Weezy” alieleza kwamba atahakikisha anajituma kwa kadri ya uwezo wake ili kupumzika atakapotimiza miaka 35. “Hiki ndicho kinachotokea unapofanya kazi sana.Watu wanadhani kwamba unaposema unafanya kazi sana ni kwamba unafanya kazi masaa mawili ya ziadaHaya ni maisha yangu, “alisema. “Ndio maana kustaafu katika umri wa miaka 35 ni sawa sawia kabisa kwangu”
Wakati wasanii wenzake kadhaa waliwahi kutangaza kustaafu na kisha kurudi kwenye game ,kama vile Jay-Z, Lil Wayne anaweka bayana kwamba yeye hatanii anaposema hivyo. “Huu ni mpango madhubuti kabisa na nitautekeleza, ”
Alipoulizwa kama ana mpango wa kuendelea kupata watoto wengine, rapper huyo aliweka wazi kwamba hana mpango huo,”Hapana,nipo sawa kwa sasa.Nina watoto wanne na nadhani wananitosha kwa wakati huu”
Hivi sasa Lil Wayne yupo katika tour “I am Music II tour” pamoja na Nicki Minaj, Rick Ross na Travis Barker na anatarajiwa kuachia album yake mpya ya The Carter IV tarehe 16 Mei mwaka huu.

No comments:

Post a Comment