.

Wednesday, April 27, 2011

MAWAZIRI TANZANIA: UNAONAJE UTENDAJI WAO...SO FAR?

Msomaji mwenzetu mmoja hapo jana aliomba kuona picha ya Baraza la Mawaziri la sasa baada ya kuona picha ya Baraza la Kwanza la Mawaziri baada ya Muungano katika post iliyopo hapo chini inayomzungumzia Oscar Kambona na Wikipedia.
Kwa bahati mbaya,hatuna picha ya Baraza la Mawaziri lililopo madarakani hivi sasa wakiwa wamesimama au kuketi pamoja. Badala yake tunayo picha hii ambayo tuliitengeneza wenyewe ya Baraza la Mawaziri lililopo madarakani.Kuna fununu kwamba siku si nyingi,Rais Kikwete atafanya mabadiliko katika baraza la mawaziri lililopo.
Sasa badala ya kuweka tu picha na kusema “pichani ni Baraza la Mawaziri na kisha kutoka kushoto kwenda kulia ni yule na yule na yule’,nadhani ni wakati muafaka tukajiuliza,Je unaonaje utendaji wa Mawaziri hawa mpaka hivi sasa?Yupi ambaye unaona anafanya kazi yake ipasavyo na yupi analegalega au kutowajibika kabisa.

No comments:

Post a Comment