.

Wednesday, May 18, 2011

"JAMANI ETI MWISHO WA DUNIA UMEFIKA?"

Mchungaji wa kanisa moja huko California Marekani, Harold Camping, ametabiri kuwa Mei 21,2011 saa moja kamili usiku mwisho wa dunia, na huenda tusiione tena jumapili ya wiki ijayo, kwani dunia itakuwa imefika mwisho  wake siku hiyo ya Jumamosi.

Mchungaji Camping kwa kutumia mahesabu ya tarehe na mafunzo ya Biblia, ametabiri kuwa kiama kitakuwa jumamosi, na miezi mitano baadae kwenye tarehe 21 Oktoba, Mungu ataiteketeza dunia.
Mchungaji Camping ambaye anamiliki radio ya Christian Family Network yenye mtandao mkubwa sana nchini humo na sehemu zingine duniani ikiwa inarusha matangazo kwa lugha zaidi 48 zikiwemo lugha kutoka Afrika Kusini.
Camping mwenye umri wa miaka 89 ana wafuasi wengi sana duniani na sasa anaendesha kampeni kubwa kuwajulisha watu kuhusu mwisho wa dunia hapo Mei 21.

No comments:

Post a Comment