.

Friday, July 15, 2011

PATTY LABELLE




Jina lake halisi ni Patricia Louise Holt Edwards alizaliwa miaka 67 iliyopita ni mwanamama mwimbaji kutoka nchini Marekani,mwandishi pamoja na mwigizaji pia.Patty Labelle alitumia miaka 16 kama mwimbaji kiongozi wa kundi la  Patti LaBelle and the Bluebelles ambalo lilibadilisha jina na kuitwa Labelle mwanzoni mwa miaka ya 70 na kutoa nyimbo maarufu ya disco ilipewa jina la "Lady Marmalade".






Mwanamama huyo aliolewa mwaka na mume wake Armstead Edwards Julai 1973 na kumzaa mtoto wao wa kwanza na wa pekee Zuri Kye Edwards na mwishoni mwa mwaka 1970 Labelle na mume wake Edwards waliasili watoto Stanley na Todd baada ya mama yao kufariki kwa ugonjwa wa saratani.




Patty Labelle ameendelea kukonga nyoyo za watu kwa vibao vyake vikali vya miaka hiyo vinavyotamba hadi leo na huchoki kusikia kwenye masikio yako kama ''If You Asked Me To'',"Stir It Up" na "New Attitude" na nyimbo nyingine kama "You Are My Friend" na "Love, Need and Want You" na ameshawahi kupata tuzo nyingi kupitia fani yake ikiwemo hivi karibuni alipopata tuzo ya Life Time Archivement Award ya BET.

No comments:

Post a Comment