.

Friday, July 15, 2011

CHRIS BROWN AVILAUMU VYOMBO VYA HABARI




Nyota wa RnB Chris Brown amevitupia lawama vyombo vya habari kwa kutengeneza stori inayomtuhumu kuonyesha ishara ya kuwadhihaki mashoga katika mchezo wa mpira wa kikapu uliofanyika hivi karibuni.


Chris Brown akitoa shukrani katika tuzo za BET

Nyota huyo anayejaribu kujenga wasifu wake kwa jamii tangu tukio la mwaka 2009 la kumtwanga aliyekuwa mpenzi wake Rihanna, inadaiwa alishindwa kudhibiti hasira zake wakati akicheza mpira kwenye gym jijini Los Angeles na kuonyesha ishara ya kudhihaki mashoka kwa mchezaji mwingine.

Kwa mujibu wa jarida moja nchini Marekani, Brown alitoa lugha chafu na kumdhihaki mpinzani wake kwa kutembea kishoga pamoja na kumuonyesha ishara kuwadhihaki mashoga.

No comments:

Post a Comment