.

Sunday, May 15, 2011

MJUE TAJIRI MKUBWA DUNIANI.

Carlos Slim, tajiri mkubwa kabisa duniani, kwa mara nyingine tena ameendelea kutete kiti chake cha mtu mwenye mavumba zaidi ya binadamu mwingine yeyote hapa duniani. Carlos ni mtu wa Mexico na ni mmiliki wa makampuni yanayojihusisha na huduma za mawasiliano.
Kwa mujibu wa jarida la Forbes ni kwamba Slim kwa mara nyingine amempiga bao mwenyekiti wa kampuni la Microsoft, Bill Gates, ambaye ndiye alikuwa tajiri mkubwa kwa kitambo kirefu kabla ya kubwagwa na Slim miaka michache iliyopita.
Jarida la Forbes linasama kwa takwimu zao inaonekana Slim amejiongezea utajiri wake kwa karibu asilimia 40 zaidi. Thamani ya utajiri wake imeongezeka toka dolari bilioni 20.5 hadi dolari bilioni 74, huku akimwacha Gates katika nafasi ya pili akiwa na dolari bilioni 56 mchagoni.
Forbes wanendelea kutwambia kwamba mwaka huu kumekuwa na ongezeko la idadi ya mabilionea wapya 200. Sita kati ya mabilionea hawa ni wawekezaji katika hisa za kampuni la Facebook, akiwamo mwanzilishi wa kampuni hilo, Mark Zukcerberg.
Dustin Moskovitz ndiye bilionea mdogo kuliko wote duniani, akiwa na umri wa miaka 26 tu, na ni mwekezaji katika hisa za kampuni la Facebook.
Mwanzilishi wa kampuni la  Ikea, Ingvar Kamprad, ndio bilionea aliyepoteza fedha nyingi kwa mwaka huu. Forbes wameshudia utajiri wake ukiporomoka toka dolari bilioni 17 kibindoni hadi bilioni 6 mchagoni.
Inasemekana utajiri wa pamoja wa mabilionea wote hawa umefikia dolari trilioni 4.5, wamevunja rekodi.
Ifuatayo ni ordha ya mabilionea hawa wa dunia:

No comments:

Post a Comment