.

Tuesday, August 2, 2011

MWANAMKE MTANZANIA ASHITAKIWA KUMILIKI MTUMWA.............


Mwanake mmoja nchini Uingereza Bi. Rebbeca Balira, mwenye umri wa miaka 47 aishie jijini London ameshtakiwa kwa kosa la kum-miliki msichana wa kazi aitwae Methodia Mathias mwenye umri wa miaka 21 kama mtumwa.

Bi Rebecca Balira ni scientist (HIV expert) anayeaminika kwenye kituo mashuhuri duniani cha utafiti wa magonjwa ya Ukimwi na magonjwa ya kitropical kilichoko jijini London.


Bi Rebecca Balira ameshtakiwa kwenye Mahakama ya mjini London (Southwark Crown Court) kwa makosa mengi yakiwemo;


1. Kum-miliki msichana kinyume cha sheria (kumfanya mtumwa).

 2. Pia bi Rebecca Balira alimnyang'anya passport msichana wake wa kazi na kuificha,

 3. kumfanyisha kazi nyingi bila kumpa muda wa kupumzika (break), kumfanyisha kazi masaa mengi kuanzia alfajiri saa 11 hadi usiku saa 6.

 4. kumfanyisha kazi bila malipo,

 5. kumnasa mabao mashavuni/usoni na kumsina, kumfokea muda wote na mengine mengi.

Kutokana na uchunguzi uliofanywa inasemekana Rebecca Balira alimuahidi mfanyakazi huyo Methodia Mathias kumpatia mshara wa pound £96 za kiingereza (karibia sawa na 250,000 ya Tanzania) kipindi alipokuwa anamchukua nchini Tanzania kumleta Uingereza pesa ambayo ni ndogo sana kwa mfanyakazi wa ndani wa Uingereza kwani ni sawa na pesa ya malipo yake ya siku mbili na sio siku 30. Kwa sheria za Uingereza, unapoajiri msichana wa kazi ni lazima alipwe kiwango kilichopangwa na serikali.

Polisi walipewa taarifa ya kisanga hiki na mtu ambaye alikuwa karibu, mapolisi waliamua kwenda kufatilia walipopewa taarifa na walipofika nyumbani kwa Rebecca na kumhoji alikana kosa na kusingizia kuwa Methodia Mathias ni mtoto wa nduguye. Mapolisi waliamua kumpeleka mahakamani kumfungulia mashitaka kutokana na ushahidi wa mazingira waliyoyakuta mule ndani kwa Rebecca kwani msichana wa kazi hakuwa na chumba chake maalumu cha kulala bali alilala kitanda kimoja na mtoto wa kiume wa Rebecca.

No comments:

Post a Comment