.

Wednesday, July 20, 2011

AWAUA WAZAZI WAKE NA KUANGUSHA PARTY NYUMBANI



Kijana mmoja wa kiume katika jimbo la Florida nchini Marekani anatuhumiwa kuwauwa wazazi wake kwa kuwapiga nyundo na kisha akafanya tafrija yaani party amefikishwa mahakamani.

Kijana huyo ambaye ametambuliwa kwa jina la Tyler Hadley, mwenye umri wa miaka 17 anatuhumiwa kuwauwa wazazi wake Blake na Mary-Jo Hadley siku ya jumamosi na kisha akawafuingia miili hiyo chumbani na kuwaalika wageni  katika hafla hiyo.

Amefunguliwa mashitaka kama mtu mzima lakini hatahukumiwa kifungo cha kifo kwa kuwa umri wake ni mdogo na chanzo cha mauaji hayo bado hakijajulikana.

No comments:

Post a Comment